• Contact us |
    • FAQ |
    • Opinions |
Health System Strengthening Resource Center

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Health System Strengthening Resource Center

  • Home
  • About Us
    • Background
    • Mission & Vission
    • Objective
    • Roles & Function
    • HSSRC Team
  • Administration
  • Services
    • Training
    • Research & Consultancy
    • eLibrary
  • Publications
    • Guidelines
      • Health Financing
      • Information Managment
      • Service Delivery
        • Curative
        • Preventive
        • Medicine logistics
        • Infrastructure
        • Social Welfare
        • Nutrition
      • Medical Products,Vaccines & Technology
      • Leadership / Governance
      • Human Resources
    • Reports
      • National Survey Reports
      • Financial & Audit Reports
      • Health Sector Reports
      • International Reports
    • Circulars
    • Polices
    • Presentations
    • Journal articles
    • Acts and Regulations
      • Health Related Acts
      • Non Health Related Acts
  • Media Center
    • News
    • Announcements
    • Gallery
    • Videos
  • Take Actions
    • Financing
    • Service Delivery
    • Human Resouces
    • Leadership / Governance
    • Infrastructure
    • Information Managment
    • Medical Products,vaccine & Technology
  • Submit Innovation
  • Conferences
    • Annual Medical Meetings

Mtaka awapa somo Waganga wa Mkoa na Wilaya

Posted on: August 21st, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe Antony Mtaka amewataka Waganga Wakuu wa Mikoa na Wilaya kuahikikisha wanatumia taaluma yao katika kuleta maendeleo kwa jamii ili kuwasaidia wananchi maskini.

Ameyasema hayo wakati akifunga Mkutano Mkuu wa Wanganga Wakuu wa Mikoa na Wilaya leo uliofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa LAPF Jijini Dodoma.

Mhe Mtaka amewataka Waganga hao kuhakikisha wanafanyakazi kwa kuzingatia sheria, taratibu na weledi weledi wa hali ya juu kwa kutetea kada ya madaktari nchini ili kuongeza ufanisi na kuleta maendeleo nchini.

“Inasikitisha kuona Mganga Mkuu wa Mkoa na Wilaya yupo halafu unakuta kituo cha afya kimejengwa hovyo, mpaka viongozi waje ndio wanagundua kasoro, ukiona hivyo inaonyesha hautoshi katika uongozi.” Anasema Mtaka.

Amesema kuwa Serikali imewekeza fedha nyingi katika sekta ya Afya hivyo ni wajibu wao kuhakikisha wanafikia malengo ya kuleta mabadiliko katika sekta ya afya ili kumsaidia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli katika suala zima kusaidia jamii maskini nchini.  

Mhe. Mtaka amesema Serikali imewekeza fedha nyingi katika Sekta ya afya hivyo ni wajibu wa kila kiongozi kusimamia kwa weledi ili kuleta mabadiliko na kupunguza kero za afya nchini.

Akisistiza katika kuwekeza kwa wataalam wa afya Mhe Mtaka amewataka Waganga hao kuhakikisha wanaridhisha taalum hiyo kwa wataalam wapya wa afya ili iweze kuwa endelevu na kuwataka kusimamia maadili katika utendaji kazi.

“Tuwekeze  kwa wataalam wa afya kwa kuwasomesha na kuwaridhisha taaluma hiyo ili vizazi vijavyo viweze kufanya kazi kwa uadilifu na uaminifu katika utoaji wa huduma za afya nchini ‘’Anasema Mtaka.

Amesema kuwa kama hakuna maadili katika sekta ya afya taaluma hiyo haitakuwa na manufaa kwa jamii, hivyo amewataka kuhakikisha wanasimamia maadili kwa watumishi wa sekta ya afya nchini.

Aidha ameawataka kuhakikisha kuwa wanakuwa chachu ya maendeleo katika jamii kwa kutumia taaluma yao katika kutoa ushauri ili mabadiliko hayo yafanyike kuanzia ngazi ya vijiji, kata na taifa kwa ujumla.

Wakati huohuo Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa anayeshughulikia afya Dkt. Zainabu Chaula amewataka watumishi wa sekta ya afya kushirikiana katika kazi ili kuleta maendeleo na kutoa huduma bora za afya.

“Wataalam wote wanawajibu wa kuwajibika ipasavyo katika utoaji wa huduma kwa jamii ili kuweza kutekeleza ilani ya Chama cha Mapinduzi ya kuhakikisha sekta ya afya inatoa huduma stahiki kwa jamii.

Aidha amesema kuwa hakutakuwa na mafanikio kama hakutakuwa na umoja na mshikamano katika utendaji kazi, hivyo amewataka kuhakikisha kuwa wanafanyakazi katika umoja na kuleta maendeleo.



Announcements

  • Call for applications for the TDR Postgraduate Training Scholarship in Implementation Science for the 2022 Academic Year (starting January 2022) May 16, 2021
  • Free Online IMF-Public Financial Management Course May 18, 2021
  • ARISE-PP Grants: Call for Expressions of Interest June 25, 2021
  • APPLICATION FOR THE SWEEDEN 2021 SCHOLARSHIP PROGRAM IS OUT. July 12, 2021
  • View All

Latest News

  • TUNZENI VIFAA VYA AFYA VILIVYONUNULIWA NA SERIKALI - DKT. MAHERA

    March 30, 2023
  • WAUGUZI NA WAKUNGA WATAKIWA KUSIMAMIA MAADILI YA KAZI

    March 13, 2023
  • DKT. DUGANGE AAGIZA UCHUNGUZI KUFANYIKA HOSPITALI YA WILAYA ARUSHA, UPOTEVU WA MAPATO NA DAWA

    March 08, 2023
  • SERIKALI KUSOGEZA HUDUMA ZA AFYA TARAFA ZOTE

    March 02, 2023
  • View All

Video

Hospitali ya Uhuru Dodoma
More Videos

Quick Links

  • elearning.moh.go.tz
  • About Us

Related Links

  • Line ministry
  • Regions
  • Councils
  • Development partners
  • Institutions & Agences
  • Development Partners Group Tanzania (DPG)

World visitors tracker

world map hits counter

Contact us

    PO-RALG

    Postal Address: 1923

    Telephone: +255 26 232 1 234

    Mobile: +255 735160210

    Email: james.tumaini@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

Writingmasterthesis.com

    • FAQ
    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.