• Contact us |
    • FAQ |
    • Opinions |
Health System Strengthening Resource Center

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Health System Strengthening Resource Center

  • Home
  • About Us
    • Background
    • Mission & Vission
    • Objective
    • Roles & Function
    • HSSRC Team
  • Administration
  • Services
    • Training
    • Research & Consultancy
    • eLibrary
  • Publications
    • Guidelines
      • Health Financing
      • Information Managment
      • Service Delivery
        • Curative
        • Preventive
        • Medicine logistics
        • Infrastructure
        • Social Welfare
        • Nutrition
      • Medical Products,Vaccines & Technology
      • Leadership / Governance
      • Human Resources
    • Reports
      • National Survey Reports
      • Financial & Audit Reports
      • Health Sector Reports
      • International Reports
    • Circulars
    • Polices
    • Presentations
    • Journal articles
    • Acts and Regulations
      • Health Related Acts
      • Non Health Related Acts
  • Media Center
    • News
    • Announcements
    • Gallery
    • Videos
  • Take Actions
    • Financing
    • Service Delivery
    • Human Resouces
    • Leadership / Governance
    • Infrastructure
    • Information Managment
    • Medical Products,vaccine & Technology
  • Submit Innovation
  • Conferences
    • Annual Medical Meetings

Sekta binafsi zatakiwa kuwekeza katika viwanda vya kutengeneza za afya.

Posted on: November 15th, 2018

Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe Josephat Sinkamba Kandege ametoa wito kwa sekta binafsi kuwekeza katika sekta ya afya  hasa kwenye viwanda vya kutengeneza  bidhaa za afya nchini.

Ameyasema hayo wakati akifunga mkutano wa Tano wa wadau wa Sekta ya afya nchini uliofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere leo jijini Dar-es-salaam.

Mhe. Kandege amesema kuwa Tanzania  kwa sasa kuna makampuni 14  yanayojishughulisha na bidhaa za afya (Dawa, Vifaa, vifaa tiba na  vitenda) yenye mtaji mdogo ukilinganisha na mahitaji ya huduma hiyo nchini hivyo ni vyema makampuni binafsi yakawekeza ili kukidhi mahitaji ya nchi.

Mhe. Kandege amewataka wawekezaji wenye nia ya dhati  kuja kuwekeza kwenye makampuni  ya kutengeneza  bidhaa za afya hasa watanzani  wenye uwezo wa kifedha  kutumia nafasi hii adimu kuwekeza nchini.

Amesema kuwa kasi ya makampuni ya wazawa kuwekeza katika viwanda vya bidhaa za afya  nchini hayaendani na uhitaji  halisi kwa sasa kwa kuwa nchi huagiza  asilimi 94 kutoka nje.

Amesema kuwa sekta ya afya ni muhimu katika jamii hivyo ni vyema  makampuni binafsi kuhakikisha wanawekeza katika katika viwanda vya madawa kwa kuwa uhitaji wa dawa nchini ni mkubwa  ukilinganisha na uzalishaji wa bidhaa hizo nchini.

Mhe. Kandege amesema kuwa Tanzania  inatumia  zaidi ya shilingi trilioni  moja ( trilioni 1 )  kila mwaka  katika masuala ya afya lakini  ni asilimia kumi ndio hutumika katika viwanda vya ndani.

Wakati huohuo Rais wa chama cha wadau wa Afya nchini  Dkt. Omary Chilo amesema kuwa lengo la mkutano huo ni kujadili changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta ya afya nchini hasa katika uwekezaji wa makampuni ya afya nchi jambo ambalo bado ni changamoto nchini Tanzania.

Amesema maendeleo ya viwanda katika sekta ya afya ni jambo la muhimu kwa kuwa teknolojia imebadilika  na magonjwa yanayobadilika  hivyo uwekezaji katika sekta afya  kutaleta mabadiliko katika utengenezaji wa  madawa jambo ambalo litahusisha utengenezaji wa vifaa tiba na kuwekeza katika rasilimali watu.

Amesema kuwepo na viwanda vya kutengeneza bidhaa za afya (Dawa,vifaa, vifaa tiba na vitenda) nchini  kutasaidia  kupunuza bei ya madawa  ambazo zitamsaidia mwananchi maskini , kuongeza ajira kwa na kuongeza ushindani  ili kuleta tija katika kukuza uchumi wa nchi katika sekta ya afya.

Aidha  amesema kuwa dunia imekuwa kama kijiji kwa kuwa hakunakitu kinachoweza kufanyika bila kuwa na takwimu sahihi, hivyo ni vyema kukawa na mkakati wa kukusanya , kuingiza  na kuifadhi na jinsi ya kutumia takwimu mbalimbali ili kuboresha afya nchini.



Announcements

  • Call for applications for the TDR Postgraduate Training Scholarship in Implementation Science for the 2022 Academic Year (starting January 2022) May 16, 2021
  • Free Online IMF-Public Financial Management Course May 18, 2021
  • ARISE-PP Grants: Call for Expressions of Interest June 25, 2021
  • APPLICATION FOR THE SWEEDEN 2021 SCHOLARSHIP PROGRAM IS OUT. July 12, 2021
  • View All

Latest News

  • TUNZENI VIFAA VYA AFYA VILIVYONUNULIWA NA SERIKALI - DKT. MAHERA

    March 30, 2023
  • WAUGUZI NA WAKUNGA WATAKIWA KUSIMAMIA MAADILI YA KAZI

    March 13, 2023
  • DKT. DUGANGE AAGIZA UCHUNGUZI KUFANYIKA HOSPITALI YA WILAYA ARUSHA, UPOTEVU WA MAPATO NA DAWA

    March 08, 2023
  • SERIKALI KUSOGEZA HUDUMA ZA AFYA TARAFA ZOTE

    March 02, 2023
  • View All

Video

Hospitali ya Uhuru Dodoma
More Videos

Quick Links

  • elearning.moh.go.tz
  • About Us

Related Links

  • Line ministry
  • Regions
  • Councils
  • Development partners
  • Institutions & Agences
  • Development Partners Group Tanzania (DPG)

World visitors tracker

world map hits counter

Contact us

    PO-RALG

    Postal Address: 1923

    Telephone: +255 26 232 1 234

    Mobile: +255 735160210

    Email: james.tumaini@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

Writingmasterthesis.com

    • FAQ
    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.