• Contact us |
    • FAQ |
    • Opinions |
Health System Strengthening Resource Center

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Health System Strengthening Resource Center

  • Home
  • About Us
    • Background
    • Mission & Vission
    • Objective
    • Roles & Function
    • HSSRC Team
  • Administration
  • Services
    • Training
    • Research & Consultancy
    • eLibrary
  • Publications
    • Guidelines
      • Health Financing
      • Information Managment
      • Service Delivery
        • Curative
        • Preventive
        • Medicine logistics
        • Infrastructure
        • Social Welfare
        • Nutrition
      • Medical Products,Vaccines & Technology
      • Leadership / Governance
      • Human Resources
    • Reports
      • National Survey Reports
      • Financial & Audit Reports
      • Health Sector Reports
      • International Reports
    • Circulars
    • Polices
    • Presentations
    • Journal articles
    • Acts and Regulations
      • Health Related Acts
      • Non Health Related Acts
  • Media Center
    • News
    • Announcements
    • Gallery
    • Videos
  • Take Actions
    • Financing
    • Service Delivery
    • Human Resouces
    • Leadership / Governance
    • Infrastructure
    • Information Managment
    • Medical Products,vaccine & Technology
  • Submit Innovation
  • Conferences
    • Annual Medical Meetings

Serikali yapongeza juhudi za usafi wa mazingira kwenye shule za Mkoa wa Manyara

Posted on: June 20th, 2020

Na Atley Kuni- MANYARA.

Serikali imepongeza juhudi za usafi wa mazingira katika shule za mkoa wa Manyara chini ya usimamizi wa uongozi wa Mkoa huo kwenye kutekeleza ajenda ya usafi mazingira katika Shule na kwenye Jamii.

Juhudi hizo zimeshuhudiwa na Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais TAMISEMI, anayeshughulikia afya, Daktari Dorothy Gwajima alipofanya ziara katika Mkoa huo akiwa na wataalam wa Ofisi hiyo kwa lengo la kujionea hali ya utekelezaji wa elimu ya afya na mazingira katika shule zinazomilikiwa na Serikali pamoja na taasisi Binafsi.

Akiwa katika shule ya kutwa ya Babati Sekondari, aliusifu uongozi wa Shule kwa kuzingatia kanuni za afya mashuleni kwa jinsi walivyoweza kuwapanga kwa nafasi wanafunzi katika Mabweni wakiwa wameacha nafasi ya kutosha kutoka kitanda kimoja na kingine pia usafi wa vyoo ukiwa wa viwango na pia wakiwa wamezingatia uwekaji wa vyombo vya maji tiririka na sabuni kila eneo la shule.

“Nimekagua hatua kwa hatua kuona jinsi gani mnatekeleza miongozo iliyotolewa na Wizara ya Afya juu ya suala la Afya Mazingira na kwa kweli sina budi kusema mmenikosha sana na hali usafi, yaani chooni ni kusafi kiasi hata huwezi kusikia harufu yoyote, mimi niwatie moyo, endeleeni na usafi huu”, alisema Dkt. Gwajima.

Akiwa katika Shule hiyo ya Babati Day, yeye pamoja na mtaalamu wa lishe kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI, walikula chakula kilichokuwa kimeandaliwa kwa ajili ya Wanafunzi kwa lengo la kujionea ubora wa chakula kinachotumiwa na wanafunzi hao.

“Wali huu ni mtamu sana, hivi haya maharage mmenunua wapi”, alisikia Naibu Katibu Mkuu, huku akipeleka Kongole kwa mpishi wa shule hiyo kwa kuwajali wanafunzi na kuwataka kujizatiti katika suala la mboga za majani kwa kuhakikisha Uongozi wa Shule unaratibu kulima mboga mboga kwani wana maeneo mazuri yanayoweza kustawisha mboga za majani kwa wingi.

Akiwa katika Shule ya Sekondari Singe na Hayatul Islamiya, ambazo zote zinamilikiwa na taasisi za dini, Naibu Katibu Mkuu hakusita kuonesha furaha yake kwa namna taasisi hizo zilivyoweza kutekeleza kwa vitendo maelekezo ya Serikali hususan kwenye kipindi hiki cha mlipuko wa ugonjwa wa Corona, ambapo aliweza kujionea Miongozo ikiwa imebandikwa katika shule hizo, lakini pia wanafunzi wakiwa wamechukuwa tahadhari zote za kujilinda dhidi ya maradhi ya ugonjwa huo.

Kwa upande wao uongozi wa shule hizo kwa Nyakati tofauti, waliihakikishia Serikali kuendeleza ushirikiano wao wa karibu katika kutekeleza maagizo yote na miongozo inayotolewa na Serikali katika kutekeleza wajibu wao.

“Ndugu Naibu Katibu Mkuu, naomba nikuhakikishie kuwa, sisi kama shule za taasisi za dini, tutaendelea kushirikiana na Serikali bega kwa bega na kufuata maagizo yote yanayotolewa kwa mustakabali mzuri na thabiti wa afya za Wanafunzi wetu na na ufanisi wa Serikali yetu. Alisema Mkuu wa Shule hiyo Padre Joseph Sakilu.

Naye Mkuu wa Shule ya Hayatul Islamiya Hussen Mwinami alisema, kama shule tayari walishawapokea wanafunzi wote wa kidato cha sita watakaoanza mitihani yao mwishoni mwa mwezi Juni, 2020, lakini pia wamesha weka mazingira rafiki na salama kwa ajili ya kuwapokea wanafunzi watakaoanza masomo yao tarehe 29 Juni, 2020.

Akiongea wakati wa ziara hiyo Afisa Elimu wa Mkoa huo, Bw. Samson Hango, alimuahidi Naibu Katibu Mkuu kuendelea kushirikiana katika utendaji kazi na wataalam wa Afya na taasisi zote zenye mapenzi mem ana suala la usafi wakati wote ili kuhakikisha mkoa huo unaendelea kuwa kinara kwenye suala la usafi wa mazingira katika nyanja zote huku wakiahidi kufuatilia na kuhakikisha kasoro ndogo ndogo zote zilizobainika wakati wa ziara zinatatuliwa mara moja.

Ujumbe huo kutoka Ofisi ya Rais–TAMISEMI, ukiongozwa na Naibu Katibu Mkuu, ulifanya ziara ya kutembelea na kukagua Shule za Sekondari zilizopokea wanafunzi wa kidato cha sita wanaotarajiwa kuanza mitihani yao ya kuhitimu kuanzia Juni, 29, 2020. Katika ziara hiyo Shule na Vituo vya afya vilivyofikiwa na ziara hiyo ni pamoja na Aldergate Sekondari, Babati Day Sekondari na Kituo cha Afya Mutuka, maeneo mengine ni Singe Sekondari, Bonga Sekondari pamoja na Hayatul Islamiya Sekondari.

MWISHO.

Announcements

  • Call for applications for the TDR Postgraduate Training Scholarship in Implementation Science for the 2022 Academic Year (starting January 2022) May 16, 2021
  • Free Online IMF-Public Financial Management Course May 18, 2021
  • ARISE-PP Grants: Call for Expressions of Interest June 25, 2021
  • APPLICATION FOR THE SWEEDEN 2021 SCHOLARSHIP PROGRAM IS OUT. July 12, 2021
  • View All

Latest News

  • TUNZENI VIFAA VYA AFYA VILIVYONUNULIWA NA SERIKALI - DKT. MAHERA

    March 30, 2023
  • WAUGUZI NA WAKUNGA WATAKIWA KUSIMAMIA MAADILI YA KAZI

    March 13, 2023
  • DKT. DUGANGE AAGIZA UCHUNGUZI KUFANYIKA HOSPITALI YA WILAYA ARUSHA, UPOTEVU WA MAPATO NA DAWA

    March 08, 2023
  • SERIKALI KUSOGEZA HUDUMA ZA AFYA TARAFA ZOTE

    March 02, 2023
  • View All

Video

Hospitali ya Uhuru Dodoma
More Videos

Quick Links

  • elearning.moh.go.tz
  • About Us

Related Links

  • Line ministry
  • Regions
  • Councils
  • Development partners
  • Institutions & Agences
  • Development Partners Group Tanzania (DPG)

World visitors tracker

world map hits counter

Contact us

    PO-RALG

    Postal Address: 1923

    Telephone: +255 26 232 1 234

    Mobile: +255 735160210

    Email: james.tumaini@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

Writingmasterthesis.com

    • FAQ
    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.