• Contact us |
    • FAQ |
    • Opinions |
Health System Strengthening Resource Center

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Health System Strengthening Resource Center

  • Home
  • About Us
    • Background
    • Mission & Vission
    • Objective
    • Roles & Function
    • HSSRC Team
  • Administration
  • Services
    • Training
    • Research & Consultancy
    • eLibrary
  • Publications
    • Guidelines
      • Health Financing
      • Information Managment
      • Service Delivery
        • Curative
        • Preventive
        • Medicine logistics
        • Infrastructure
        • Social Welfare
        • Nutrition
      • Medical Products,Vaccines & Technology
      • Leadership / Governance
      • Human Resources
    • Reports
      • National Survey Reports
      • Financial & Audit Reports
      • Health Sector Reports
      • International Reports
    • Circulars
    • Polices
    • Presentations
    • Journal articles
    • Acts and Regulations
      • Health Related Acts
      • Non Health Related Acts
  • Media Center
    • News
    • Announcements
    • Gallery
    • Videos
  • Take Actions
    • Financing
    • Service Delivery
    • Human Resouces
    • Leadership / Governance
    • Infrastructure
    • Information Managment
    • Medical Products,vaccine & Technology
  • Submit Innovation
  • Conferences
    • Annual Medical Meetings

Dkt. Gwajima Apokelewa TAMISEMI, Mwenyewe atoa neno

Posted on: January 14th, 2019

Watumishi wametakiwa kuwa na uelewa wa kazi wanazofanya kuanzia ngazi ya kijiji hadi Taifa ili kuimarisha uratibu mzuri, uwazi, utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku na kufanya watanzania wajivunie uwepo wao katika nafasi hizo.

Hayo yamebainishwa leo na Naibu Katibu Mkuu (Afya) Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI), Dkt.Dorothy Gwajima wakati wa kikao chake cha kwanza baada ya mapokezi yaliyohudhuriwa na menejimenti na watumishi wa Ofisi ya Rais – TAMISEMI jijini Dodoma leo.

“Sisi watumishi ndio ramani ya watanzania kuweza kufikia chachu ya maendeleo ya nchii hii, hivyo tukiratibu na kutekeleza majukumu yetu kwa ufasaha ni haki yetu kupata matokeo chanya ya maendeleo ya nchi hii” Amesema Dkt.Gwajima.

Dkt.Gwajima amesema lazima serikali ijenge mfumo mzuri wa uratibu na utekelezaji wa majukumu yake kuanzia ngazi ya kijiji hadi Taifa kwani ndio njia stahiki ya kuweza kupata Tanzania yenye maendeleo na kufanya watanzania kujifunia Utanzania wao.

Akiongea katika kikao cha menejimenti ya Ofisi ya Rais TAMISEMI wakati wa kumkaribisha Naibu Katibu Mkuu (Afya) Dorothy Gwajima, Kaimu Katibu Mkuu Tixson Nzunda Ofisi ya Rais - TAMISEMI), amesema ili mtumishi wa Umma aweze kutimiza majukumu yake ya kila siku ni lazima atambue kuwa yeye ni wakili wa anaowahudumia, mratibu wa matokeo chanya, awe mcheshi kwa jamii anayoihudumia na yeye ajihisi ni sehemu moja wapo ya jamii hiyo.

Katika hatua nyingine kwenye kikao maalum na watumishi wa Idara ya Afya, Dkt. Gwajima amewaasa watumishi wa Idara ya Afya Ofisi ya Rais -TAMISEMI kuuvaa uhusika wa jamii wanayoitumikia katika kutekeleza majukumu yao ili kupata chachu ya kufanya kazi kwa ufanisi, juhudi na kutoa huduma bora kwa watanzania.

Naye Mkurugenzi wa Idara ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe Ofisi ya Rais - TAMISEMI, Dkt. Ntuli Kapologwe amempongeza Dkt. Gwajima kwa kuteuliwa kushika nafasi hiyo kwa niaba ya Idara yake ambapo ameahidi watampa ushirikiano wa kutosha ili kuhakikisha watanzania wanapata huduma bora za afya kuanzia ngazi ya kijiji hadi Taifa na kwamba wapo tayari kupokea maelekezo yote ya Serikali.

Akitoa neno la shukrani kwa niaba ya wakurugenzi na watumishi wa Ofisi ya Rais - TAMISEMI, Mkurugenzi wa Kitengo cha Ukaguzi na Ufuatiliaji wa Fedha katika Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa OR-TAMISEMI Miriam Mmbaga amesema kuwa ameguswa na mfumo aliokuja nao Dkt. Gwajima wa kutaka uratibu, uwazi, utekelezaji na ugatuzi wa madaraka kuanzia ngazi ya kijiji mpaka Taifa na kwamba utaleta chachu ya matokeo bora katika kutekeleza majukumu yao.

Dkt.Gwajima ameteuliwa na Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hapo jana kuwa Naibu Katibu Mkuu (Afya) Ofisi ya Rais TAMISEMI ambapo kabla ya uteuzi huo alikuwa Mkurugenzi wa Tiba wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto.

Announcements

  • Call for applications for the TDR Postgraduate Training Scholarship in Implementation Science for the 2022 Academic Year (starting January 2022) May 16, 2021
  • Free Online IMF-Public Financial Management Course May 18, 2021
  • ARISE-PP Grants: Call for Expressions of Interest June 25, 2021
  • APPLICATION FOR THE SWEEDEN 2021 SCHOLARSHIP PROGRAM IS OUT. July 12, 2021
  • View All

Latest News

  • TUNZENI VIFAA VYA AFYA VILIVYONUNULIWA NA SERIKALI - DKT. MAHERA

    March 30, 2023
  • WAUGUZI NA WAKUNGA WATAKIWA KUSIMAMIA MAADILI YA KAZI

    March 13, 2023
  • DKT. DUGANGE AAGIZA UCHUNGUZI KUFANYIKA HOSPITALI YA WILAYA ARUSHA, UPOTEVU WA MAPATO NA DAWA

    March 08, 2023
  • SERIKALI KUSOGEZA HUDUMA ZA AFYA TARAFA ZOTE

    March 02, 2023
  • View All

Video

Hospitali ya Uhuru Dodoma
More Videos

Quick Links

  • elearning.moh.go.tz
  • About Us

Related Links

  • Line ministry
  • Regions
  • Councils
  • Development partners
  • Institutions & Agences
  • Development Partners Group Tanzania (DPG)

World visitors tracker

world map hits counter

Contact us

    PO-RALG

    Postal Address: 1923

    Telephone: +255 26 232 1 234

    Mobile: +255 735160210

    Email: james.tumaini@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

Writingmasterthesis.com

    • FAQ
    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.