• Contact us |
    • FAQ |
    • Opinions |
Health System Strengthening Resource Center

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Health System Strengthening Resource Center

  • Home
  • About Us
    • Background
    • Mission & Vission
    • Objective
    • Roles & Function
    • HSSRC Team
  • Administration
  • Services
    • Training
    • Research & Consultancy
    • eLibrary
  • Publications
    • Guidelines
      • Health Financing
      • Information Managment
      • Service Delivery
        • Curative
        • Preventive
        • Medicine logistics
        • Infrastructure
        • Social Welfare
        • Nutrition
      • Medical Products,Vaccines & Technology
      • Leadership / Governance
      • Human Resources
    • Reports
      • National Survey Reports
      • Financial & Audit Reports
      • Health Sector Reports
      • International Reports
    • Circulars
    • Polices
    • Presentations
    • Journal articles
    • Acts and Regulations
      • Health Related Acts
      • Non Health Related Acts
  • Media Center
    • News
    • Announcements
    • Gallery
    • Videos
  • Take Actions
    • Financing
    • Service Delivery
    • Human Resouces
    • Leadership / Governance
    • Infrastructure
    • Information Managment
    • Medical Products,vaccine & Technology
  • Submit Innovation
  • Conferences
    • Annual Medical Meetings

Dkt. Magembe asimama kidete Mapato, huduma kinga

Posted on: May 25th, 2021

Na Mwandisi wetu DAR ES SALAAM

NAIBU Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI, anayeshughulikia Afya Dkt. Grace Magembe, amewataka watendaji katika Mkoa wa Dar es Salaam, kuwekeza zaidi katika suala la Afya kinga sambamba na kutilia mkazo wa ukusanyaji wa mapato kwenye vituo vya katolea huduma.

Dkt. Magembe ametoa maelekezo hayo muda mfupi, mara baada yakufanya ziara ya kikazi katika Hospitali ya Wilaya ya Kigamboni na kukagua shughuli za kiutendaji kwenye Hospitali hiyo kisha kufanya mkutano wa pamoja ulio wakutanisha watendaji wa Mkoa na kutoka Halmashauri zote za Mkoa wa Dar es Salaam.

 “Nataka mhahakikishe mnafuatilia utoaji wa huduma za kinga na tiba kwenye maeneo yenu, lakini sula lingine ni usimamiaji wa karibu wa mapato na matumizi ya vituo vya tiba pamoja na vyanzo vingine vyote vya mapato” Amesema Magembe.

Dkt. Magembe amesema, Mkoa wa Dar es Salaam, ni lazima asilimia 60 ya mapato ya ndani yaelekezwe kwenye miradi ya maendeleo inayoonekana kwa macho na yenye matokeo chanya katika kutatua   changamoto za wananchi.

Kuhusiana na utatuzi wa kero kwa wananchi Dkt. Magembe amewaagiza watendaji hao, kuhakikisha wanaweka utaratibu mzuri wa kupokea kero za wananchi ikiwepo masanduku ya maoni pamoja na namba za simu za viongozi zibandikwe kwenye mbao za matangazo maeneo ya kutolea huduma sehemu za wazi.

Naibu katibu mkuu ametumia nafasi hiyo kuwaagiza wakurugenzi wote kufanya ukaguzi kwenye vituo vya tiba, na maeneo yote yanayokusanya fedha za serikali na kuangalia kama kuna matumizi ya fedha yamefanyika kabla ya fedha hizo kuwasilishwa benki, aidha watakao bainika kufanya hivyo wachukuliwe hatua kwa mujibu wa sheria.

Naibu Katibu Mkuu huyo ambaye yupo katika ziara ya kikazi kwenye Mkoa huo, amewaagiza waganga wakuu wa Mikoa kote nchini, kuhakikisha wanawasilisha taarifa za vizazi na vifo vya wajawazito na watoto wachanga kwenye vikao vya menejimenti vya Sekreatriati za mikoa na waganga wakuu wa halmashauri kufanya hivyo kwenye vikao vya menejimenti ndani ya halmashauri ili kuwa na uelewa wa pamoja katika kuchukua hatua za haraka za kiutendaji.

Katika ziara hiyo, ambayo ilikwenda sambamba na mafunzo kwa Wakurugenzi yaliyo endeshwa na Dkt. Grace, Watendaji hao wamempongeza kwa hatua hiyo, kwani imewasaidia kujua mambo mengi hasa katika utaratibu wa utoaji wa huduma za afya, na katika kuhitimisha Naibu Katibu Mkuu amemuelekeza Mfamasia katika Halmashauri ya Kigamboni kuendeleza elimu hiyo.

Hii ni ziara ya kwanza kwa Naibu Katibu Mkuu, toka ateuliwe kushika wadhifa huo mapema mwaka huu, akichukua nafasi iliyo achwa wazi na Dkt. Dorothy Gwajima, ambaye kwa sasa ni Waziri wa Afya.

MWISHO

  

Announcements

  • Call for applications for the TDR Postgraduate Training Scholarship in Implementation Science for the 2022 Academic Year (starting January 2022) May 16, 2021
  • Free Online IMF-Public Financial Management Course May 18, 2021
  • ARISE-PP Grants: Call for Expressions of Interest June 25, 2021
  • APPLICATION FOR THE SWEEDEN 2021 SCHOLARSHIP PROGRAM IS OUT. July 12, 2021
  • View All

Latest News

  • TUNZENI VIFAA VYA AFYA VILIVYONUNULIWA NA SERIKALI - DKT. MAHERA

    March 30, 2023
  • WAUGUZI NA WAKUNGA WATAKIWA KUSIMAMIA MAADILI YA KAZI

    March 13, 2023
  • DKT. DUGANGE AAGIZA UCHUNGUZI KUFANYIKA HOSPITALI YA WILAYA ARUSHA, UPOTEVU WA MAPATO NA DAWA

    March 08, 2023
  • SERIKALI KUSOGEZA HUDUMA ZA AFYA TARAFA ZOTE

    March 02, 2023
  • View All

Video

Hospitali ya Uhuru Dodoma
More Videos

Quick Links

  • elearning.moh.go.tz
  • About Us

Related Links

  • Line ministry
  • Regions
  • Councils
  • Development partners
  • Institutions & Agences
  • Development Partners Group Tanzania (DPG)

World visitors tracker

world map hits counter

Contact us

    PO-RALG

    Postal Address: 1923

    Telephone: +255 26 232 1 234

    Mobile: +255 735160210

    Email: james.tumaini@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

Writingmasterthesis.com

    • FAQ
    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.