• Contact us |
    • FAQ |
    • Opinions |
Health System Strengthening Resource Center

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Health System Strengthening Resource Center

  • Home
  • About Us
    • Background
    • Mission & Vission
    • Objective
    • Roles & Function
    • HSSRC Team
  • Administration
  • Services
    • Training
    • Research & Consultancy
    • eLibrary
  • Publications
    • Guidelines
      • Health Financing
      • Information Managment
      • Service Delivery
        • Curative
        • Preventive
        • Medicine logistics
        • Infrastructure
        • Social Welfare
        • Nutrition
      • Medical Products,Vaccines & Technology
      • Leadership / Governance
      • Human Resources
    • Reports
      • National Survey Reports
      • Financial & Audit Reports
      • Health Sector Reports
      • International Reports
    • Circulars
    • Polices
    • Presentations
    • Journal articles
    • Acts and Regulations
      • Health Related Acts
      • Non Health Related Acts
  • Media Center
    • News
    • Announcements
    • Gallery
    • Videos
  • Take Actions
    • Financing
    • Service Delivery
    • Human Resouces
    • Leadership / Governance
    • Infrastructure
    • Information Managment
    • Medical Products,vaccine & Technology
  • Submit Innovation
  • Conferences
    • Annual Medical Meetings

Jafo awapongeza wadau wa sekta ya afya

Posted on: August 21st, 2018

Waziri wa Nchi Ofisi  ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo  amesema katika kuboresha afya kunahitajika uwepo wa wadau wengine ili waweze kuunga mkono juhudi za serikali  katika kuwahudumia wananchi kwa kuwapatia huduma wanazozihitaji kwa ulinzi wa afya zao.

Akifunga mkutano wa wadau wa maendeleo katika sekta ya afya uliofanyika katika ukumbi wa Kilimani  leo Jijini Dodoma Mhe. Jafo amesema kuwa kama hakuna nia dhabiti ya kisiasa ya kiongozi wa nchi Sekta ya afya haiwezi kufanikiwa.

Amewashukuru wadau wa maendeleo katika Sekta ya Afya  kwa  kushirikiana na Serikali katika kuwekeza  kwa ajili ya kuwahudumia wananchi  maskini walipo katika Mamlaka za Serikali za Mitaa Nchini.

Amesema kuwa Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli ameamua kutekeleza Ilani ya Chama Cha mapinduzi kwa vitendo kwa kusimamia kwa dhati sekta ya afya nchini  hivyo wadau wa maendeleo katika sekta ya afya hawanabudi kuunga mkono juhudi hizo.

Akiongelea suala la utekelezaji wa majukumu kwa weledi Mhe. Jafo amesema viongozi waliopewa dhamana wana wajibu wakuhakikisha  wanakuwa mfano wa kukumbukwa na jamii katika kutimiza wajibu wao  wa kuwahudumia wananchi  maskini ambao wanahitaji huduma bora za afya nchini.

Amewapongeza  Wanganga Wakuu wa Mikoa na  Wilaya  kwa weledi na kutumia taaluma zao katika kushauri kitaalam jinsi ya kujenga vituo vya afya nchini jambo ambalo limesaidia kuhakikisha kuwa vituo vinakamilika kwa wakati na kwa gharama zilizokusudiwa na Serikali.

‘’Kwa gharama ya shilingi milioni 500 wameweza kujenga wodi ya Wazazi, Chumba cha upasuaji, maabara, chumba cha kuhifadhia maiti,  maeneo ya kutembelea wagonjwa, vichomea taka kweli  mnahitaji pongezi kwa kuwa bila maelekezo na usimamizi wenu majengo hayo yasingepatikana” Anasema Jafo

Amewaagiza kuendeleza taaluma yao kwa kufanyakazi kwa uadilifu na weledi  kwa kuwa taifa linawategemea katika kutatua changamoto za sekta ya afya na kuleta mabadiliko lengo likiwa ni kutoa huduma bora kwa jamii.

Amewataka kuhakikisha wanawasimamia wahudumu wa afya nchini na kuwataka kutumia lugha nzuri kwa wananchi ili wagonjwa waweze kuvutiwa kuja kupata huduma katika vituo vya afya nchini, na wabadilishe sekta ya afya kuwakuvifanya kuvutia  na kuwafanya wananchi  kuvutika kabla ya kupatiwa matibabu.

Mhe. Jafo amewataka kuhakikisha wanajenga imani kwa wananchi kuwa Serikali inawajali na kuwadhamini katika suala zima la utoaji huduma bora za afya nchini.

Amewashukuru wadau  wa maendeleo ya sekta ya afya nchini kwa kutenga fedha kwa ajili ya kuendeleza Sekta ya afya  na kusababisha ujenzi wa vituo vya afya unakamilika kwa wakati.

Aidha amewataka Waganga Wakuu wa Mikoa kuhakikisha  wanasimamia Hospitali   na vituo vya afya nchini  kwa kuhakikisha wanafunga mifumo ya kielektoniki ili kuweza kukusanya mapato na kupunguza ubadhilifu wa  wa mapato nchini.



Announcements

  • Call for applications for the TDR Postgraduate Training Scholarship in Implementation Science for the 2022 Academic Year (starting January 2022) May 16, 2021
  • Free Online IMF-Public Financial Management Course May 18, 2021
  • ARISE-PP Grants: Call for Expressions of Interest June 25, 2021
  • APPLICATION FOR THE SWEEDEN 2021 SCHOLARSHIP PROGRAM IS OUT. July 12, 2021
  • View All

Latest News

  • TUNZENI VIFAA VYA AFYA VILIVYONUNULIWA NA SERIKALI - DKT. MAHERA

    March 30, 2023
  • WAUGUZI NA WAKUNGA WATAKIWA KUSIMAMIA MAADILI YA KAZI

    March 13, 2023
  • DKT. DUGANGE AAGIZA UCHUNGUZI KUFANYIKA HOSPITALI YA WILAYA ARUSHA, UPOTEVU WA MAPATO NA DAWA

    March 08, 2023
  • SERIKALI KUSOGEZA HUDUMA ZA AFYA TARAFA ZOTE

    March 02, 2023
  • View All

Video

Hospitali ya Uhuru Dodoma
More Videos

Quick Links

  • elearning.moh.go.tz
  • About Us

Related Links

  • Line ministry
  • Regions
  • Councils
  • Development partners
  • Institutions & Agences
  • Development Partners Group Tanzania (DPG)

World visitors tracker

world map hits counter

Contact us

    PO-RALG

    Postal Address: 1923

    Telephone: +255 26 232 1 234

    Mobile: +255 735160210

    Email: james.tumaini@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

Writingmasterthesis.com

    • FAQ
    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.