• Contact us |
    • FAQ |
    • Opinions |
Health System Strengthening Resource Center

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Health System Strengthening Resource Center

  • Home
  • About Us
    • Background
    • Mission & Vission
    • Objective
    • Roles & Function
    • HSSRC Team
  • Administration
  • Services
    • Training
    • Research & Consultancy
    • eLibrary
  • Publications
    • Guidelines
      • Health Financing
      • Information Managment
      • Service Delivery
        • Curative
        • Preventive
        • Medicine logistics
        • Infrastructure
        • Social Welfare
        • Nutrition
      • Medical Products,Vaccines & Technology
      • Leadership / Governance
      • Human Resources
    • Reports
      • National Survey Reports
      • Financial & Audit Reports
      • Health Sector Reports
      • International Reports
    • Circulars
    • Polices
    • Presentations
    • Journal articles
    • Acts and Regulations
      • Health Related Acts
      • Non Health Related Acts
  • Media Center
    • News
    • Announcements
    • Gallery
    • Videos
  • Take Actions
    • Financing
    • Service Delivery
    • Human Resouces
    • Leadership / Governance
    • Infrastructure
    • Information Managment
    • Medical Products,vaccine & Technology
  • Submit Innovation
  • Conferences
    • Annual Medical Meetings

Komesheni ubadhilifu wa Dawa – Dkt. Gwajima

Posted on: October 29th, 2019

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Dkt. Dorothy Gwajima, amewataka Wafamasia wa Mikoa kote nchini kupambana na kukomesha watu wanaofanya ubadhilifu wa dawa zinazotolewa na serikali kwenda kwenye sehemu za kutolea huduma za afya sambamba na kutafsiri falsafa ya hapa kazi tu kwa vitendo.

Akizungumza katika kikao kazi cha wataalam hao kinachofanyika mjini Dodoma, alisema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ametekeleza vema ilani ya Chama cha Mapinduzi kwakuijali na kuipa kipaumbele sekta ya afya na ndio maana katika mwaka wa fedha 2019/20 serikali imepitisha bajeti ya Shilingi bilioni 57.4 ambapo katika mgawanyo eneo la dawa ni miongoni mwa vipaumbele vitatu vilivyo pewa umuhimu.

“Sasa tusimhujumu Mhe. Rais ambaye ameshafanya kazi kubwa na sisi tuliomo ndani ambao tumewekwa kusimamia tunaujuzi na utaalam sehemu ambayo yeye hawezi kuingia, watu wanaiba dawa tunawaangalia, wanaiba vitendanishi tunawaangalia, tutakuwa hatutimizi wajibu wetu kama matazamia yake naya wanachi yanavyotaka” alisema Gwajima.

Gwajima amewataka Wafamasia hao kutumia mfumo wa Ugavi wa dawa wa (elmis) ambao kimsingi taarifa zote za dawa zinaingizwa na kutumika kama muhtadha wa kuombea dawa kwa kila robo. Alisema mfamasia wa Mkoa atakuwa na wajibu wa kuhalalisha maombi ya dawa kwenda MSD kila mara, huku akiitaja mikoa ya kuanzia katika zoezi hilo ni pamoja na Singida, Dodoma, Manyara, Kagera na Geita.

“Tunataka kufanyika kwa Medicine Audit kila robo na taarifa yake kwa kila mkoa iwasilishwe OR-TAMISEMI” alisema Gwajima na kuongeza kuwa “lengo ni kuchakata taarifa za mifumo ya dawa ili kubaini kama kuna hazina ya dawa za kutosha au lah, ili kuweza kusaidia maeneo ambayo yanaupungufu wa dawa.” Alisisitiza Gwajima.

Katika hatua nyingine Gwajima alisema Serikali hivi sasa ipo katika maboresho makubwa ya mfumo wa uendeshaji wa shughuli za Afya (Government of Tanzania Health Management Information System-GoTHOMIS) ambao baada ya kukamilika kwake mfumo utatoa taarifa nyingi za makusanyo ya fedha za dawa mpaka ngazi ya mtumiaji wa mwisho.

Awali kabla yakumkaribisha Mgeni Rasmi, Mkurugenzi wa Idara ya Afya na Ustawi wa Jamii OR-TAMISEMI, Dkt. Ntuli Kapologwe, alisema Sekta ya Afya imekuwa  miongoni mwa sekta zilizo pewa kipaumbele na Mhe. Rais hivyo kama wataalam lazima tuoneshe kwa vitendo kuwa Mhe. Rais hajakosea katika hili.

“Mtakumbuka ziara ya mwanzo kabisa Mhe. Rais, alijielekeza katika sekata hii muhimu kwa mustakabali wa maendeleo nchi hasa wakati huu tunapoelekea katika uchumi wa kati ifikapo 2025. Lakini hakuishia hapo toka ameingia madarakani imeendelea kutenga fedha kwaajili ya kujenga na kukarabati vituo vya kutolea huduma za afya, ambapo katika mwaka wa fedha 2017/18 vituo vya afya 352 zikiwepo Hospitali 9, Vituo vya Afya 304 na Zahanati 39 zilikarabatiwa, lakini hivi sasa vituo vinavyo jengwa na kukarabatiwa vimefikia 470 zikiwemo hospitali 67 mpya za Halmashauri ambazo zitakuwa na idara kamili ya dawa” alisema Kapologwe.

Kikao cha Wafamasia kimetayarishwa na Ofisi ya Rais TAMISEMI kwa ushirikiano na wadau wa maendeleo, lengo likiwa nikuweka mipango ya kuhakikisha mianya ya ubadhilifu wa dawa inakomeshwa lakini pia kuweka mikakati endelevu ya upatikanaji wa dawa katika sehemu zote za kutolea huduma za afya.  

Na Atley Kuni- TAMISEMI.

Announcements

  • Call for applications for the TDR Postgraduate Training Scholarship in Implementation Science for the 2022 Academic Year (starting January 2022) May 16, 2021
  • Free Online IMF-Public Financial Management Course May 18, 2021
  • ARISE-PP Grants: Call for Expressions of Interest June 25, 2021
  • APPLICATION FOR THE SWEEDEN 2021 SCHOLARSHIP PROGRAM IS OUT. July 12, 2021
  • View All

Latest News

  • TUNZENI VIFAA VYA AFYA VILIVYONUNULIWA NA SERIKALI - DKT. MAHERA

    March 30, 2023
  • WAUGUZI NA WAKUNGA WATAKIWA KUSIMAMIA MAADILI YA KAZI

    March 13, 2023
  • DKT. DUGANGE AAGIZA UCHUNGUZI KUFANYIKA HOSPITALI YA WILAYA ARUSHA, UPOTEVU WA MAPATO NA DAWA

    March 08, 2023
  • SERIKALI KUSOGEZA HUDUMA ZA AFYA TARAFA ZOTE

    March 02, 2023
  • View All

Video

Hospitali ya Uhuru Dodoma
More Videos

Quick Links

  • elearning.moh.go.tz
  • About Us

Related Links

  • Line ministry
  • Regions
  • Councils
  • Development partners
  • Institutions & Agences
  • Development Partners Group Tanzania (DPG)

World visitors tracker

world map hits counter

Contact us

    PO-RALG

    Postal Address: 1923

    Telephone: +255 26 232 1 234

    Mobile: +255 735160210

    Email: james.tumaini@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

Writingmasterthesis.com

    • FAQ
    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.