• Contact us |
    • FAQ |
    • Opinions |
Health System Strengthening Resource Center

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Health System Strengthening Resource Center

  • Home
  • About Us
    • Background
    • Mission & Vission
    • Objective
    • Roles & Function
    • HSSRC Team
  • Administration
  • Services
    • Training
    • Research & Consultancy
    • eLibrary
  • Publications
    • Guidelines
      • Health Financing
      • Information Managment
      • Service Delivery
        • Curative
        • Preventive
        • Medicine logistics
        • Infrastructure
        • Social Welfare
        • Nutrition
      • Medical Products,Vaccines & Technology
      • Leadership / Governance
      • Human Resources
    • Reports
      • National Survey Reports
      • Financial & Audit Reports
      • Health Sector Reports
      • International Reports
    • Circulars
    • Polices
    • Presentations
    • Journal articles
    • Acts and Regulations
      • Health Related Acts
      • Non Health Related Acts
  • Media Center
    • News
    • Announcements
    • Gallery
    • Videos
  • Take Actions
    • Financing
    • Service Delivery
    • Human Resouces
    • Leadership / Governance
    • Infrastructure
    • Information Managment
    • Medical Products,vaccine & Technology
  • Submit Innovation
  • Conferences
    • Annual Medical Meetings

Rais Azindua Kituo cha Afya Mbonde, Apongeza TAMISEMI, Wizara ya Afya kwa Mshikamano

Posted on: April 4th, 2019

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Joseph Pombe Magufuli ameipongeza Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa kwa kushirikiana na Wizara ya afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa usimamizi  wenye weledi  katika ujenzi na ukarabati wa vituo vya kutolea huduma za Afya Nchini.

Ameyasema hayo leo kwenye uzinduzi wa Kituo cha Afya cha Mbonde katika Halmashauri Mji wa Masasi, Mkoani Mtwara kwa niaba ya vituo 352 vya kutolea huduma nchini ambavyo vimejengwa katika Halmashauri zote nchini.

Mhe. Magufuli amesema kuwa Serikali imetenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya kutolea huduma lakini Wizara hizo mbili zimeweza kusimamia kwa weledi utekelezaji wa ujenzi wa vituo hivyo.

“Kutengwa kwa fedha ni sula la msingi lakini usimamizi wa fedha ni suala muhimu sana hivyo  nimeridhishwa na usimamizi uliofanywa na Wizara hizi mbili  ambapo ujenzi umefanyika kwa kiwango kikubwa na  usimamizi huo unaacha alama kwa nchi na kupunguza kero za miundominu ya afya nchini” Amesema Mhe. Magufuli

Mhe. Magufuli amewapongeza watumishi wa  OR-TAMISEMI  na Wizara ya Afya kwa kujitoa kwa hali na mali katika kusimamia na kuhakikisha vituo vya afya vinakamilika kwa wakati na viwango vya juu na kuanza kutoa huduma kwa jamii ili kuwahudumia wananchi maskini nchini.

 “Panapostahili kupongezwa napongeza hadharani bila kificho na sitasubiri mpaka mtu afe, kwa kweli Wizara hizi mbili wamesimamia kazi ya ujenzi wa vituo vya afya kwa umakini mkubwa na wamefanyakazi nzuri” Amesisitiza Mhe. Magufuli

Amesema kuwa kwa gharama ya shilingi milioni 500 wameweza kujenga Wodi ya Wazazi, Jengo la Maabara, Chumba cha kuifadhia maiti,  chumba cha Mionzi na Jengo la upasuaji hivyo nimeridhishwa na matumizi ya fedha zilizotolewa na Serikali na wadau wa maendeleo katika Sekta ya afya

Mhe. Magufuli amewapongeza Wataalam wa afya nchini  kwa kufanyakazi kwa weledi na moyo wa kujitolea na kuwataka  kuendelea kutoa huduma bora kwa jamii maskini ambao ndio wenye uhitaji mkubwa wa huduma za afya nchini.

Aidha Mhe. Magufuli amefafanua kuwa gharama zilizotumika katika ujenzi wa vituo 352 ni shilingi bilioni 184 hivyo amewashukuru wananchi, wadau wa maendeleo kwa kujitoa kwa moyo  kuleta maendeleo katika Sekta ya afya nchini.

Wakati Huohuo Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo amesema kuwa sekta ya afya ni eneo linalogusa wananchi wa hali ya nchini hivyo serikali iliamua kuwekeza katika sekta ya afya ili kuleta mabadiliko katika jamii.

Amesema tangu uhuru kulikuwa na Hospitali za Serikali 77 katika Halmashauri 185,  vituo vya afya 535 ambapo viliyokuwa na uwezo wa kufanya upasuaji ni  vituo vya afya 118  hali hii ilikuwa ikisababisha vifo vya mama na mtoto pale anapohitaji kujifungua kwa njia ya upasiaji kwa kuwa walikuwa wakitembea muda mrefu kufuata huduma hizo katika Hospitali za Rufaa.

Aidha Mhe Jafo amesema katika miezi 18 ya ujenzi wa vituo vya afya nchini Serikali imeweza kufanya mapinduzi makubwa katika sekta ya afya ambapo mpaka sasa vituo 352 vimeweza kujengwa na vinaweza kufanya huduma ya upasuaji.

Announcements

  • Call for applications for the TDR Postgraduate Training Scholarship in Implementation Science for the 2022 Academic Year (starting January 2022) May 16, 2021
  • Free Online IMF-Public Financial Management Course May 18, 2021
  • ARISE-PP Grants: Call for Expressions of Interest June 25, 2021
  • APPLICATION FOR THE SWEEDEN 2021 SCHOLARSHIP PROGRAM IS OUT. July 12, 2021
  • View All

Latest News

  • TUNZENI VIFAA VYA AFYA VILIVYONUNULIWA NA SERIKALI - DKT. MAHERA

    March 30, 2023
  • WAUGUZI NA WAKUNGA WATAKIWA KUSIMAMIA MAADILI YA KAZI

    March 13, 2023
  • DKT. DUGANGE AAGIZA UCHUNGUZI KUFANYIKA HOSPITALI YA WILAYA ARUSHA, UPOTEVU WA MAPATO NA DAWA

    March 08, 2023
  • SERIKALI KUSOGEZA HUDUMA ZA AFYA TARAFA ZOTE

    March 02, 2023
  • View All

Video

Hospitali ya Uhuru Dodoma
More Videos

Quick Links

  • elearning.moh.go.tz
  • About Us

Related Links

  • Line ministry
  • Regions
  • Councils
  • Development partners
  • Institutions & Agences
  • Development Partners Group Tanzania (DPG)

World visitors tracker

world map hits counter

Contact us

    PO-RALG

    Postal Address: 1923

    Telephone: +255 26 232 1 234

    Mobile: +255 735160210

    Email: james.tumaini@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

Writingmasterthesis.com

    • FAQ
    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.