• Contact us |
    • FAQ |
    • Opinions |
Health System Strengthening Resource Center

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Health System Strengthening Resource Center

  • Home
  • About Us
    • Background
    • Mission & Vission
    • Objective
    • Roles & Function
    • HSSRC Team
  • Administration
  • Services
    • Training
    • Research & Consultancy
    • eLibrary
  • Publications
    • Guidelines
      • Health Financing
      • Information Managment
      • Service Delivery
        • Curative
        • Preventive
        • Medicine logistics
        • Infrastructure
        • Social Welfare
        • Nutrition
      • Medical Products,Vaccines & Technology
      • Leadership / Governance
      • Human Resources
    • Reports
      • National Survey Reports
      • Financial & Audit Reports
      • Health Sector Reports
      • International Reports
    • Circulars
    • Polices
    • Presentations
    • Journal articles
    • Acts and Regulations
      • Health Related Acts
      • Non Health Related Acts
  • Media Center
    • News
    • Announcements
    • Gallery
    • Videos
  • Take Actions
    • Financing
    • Service Delivery
    • Human Resouces
    • Leadership / Governance
    • Infrastructure
    • Information Managment
    • Medical Products,vaccine & Technology
  • Submit Innovation
  • Conferences
    • Annual Medical Meetings

TEHAMA kuongeza ufanisi kwa mtumishi wa afya ngazi ya Zahanati

Posted on: September 12th, 2018

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa kwa kushirikiana na Wizara ya afya, Maendeleo ya jamii, jinsia, Wazee na Watoto na Taasisi isiyo ya kiserikali ya PATH chini ya Mpango wa kuboresha Matumizi ya Takwimu za Afya (Data Use Partinership -DUP) imejiwekea mikakati ya kuongeza ufanisi katika utoaji huduma ya Afya kwa kuiweka Mifumo ya TEHAMA katika ngazi ya huduma ya Afya ya Msingi ili Wananchi waweze kupata huduma bora za afya.

Akitoa mada katika kikao kazi cha kuimarisha mifumo ya TEHAMA inayotumika katika Ngazi ya vituo vya afya kilichofanyika katika ukumbi wa NIMR, Jijini Dar-es-salaam Bi. Sultana Seif Afisa TEHAMA kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya jamii, jinsia, Wazee na Watoto amesema ili kumuwezesha mtumishi wa afya ngazi ya zahanati na kuweza kutoa huduma stahiki ni vyema wakafanya kazi kwa ufanini atika utendaji kazi wa kila siku kwa kutumia TEHAMA.

Bi. Sultana amesema kuwa kumekuwa na changamoto mbalimbali katika upatikanaji wa huduma sahihi na upatikanaji wa takwimu sahihi za afya kwa jamii jambo ambalo linapelekea mtumishi wa afya ngazi ya zahanati kuwa na mzigo mkubwa unaopelekea kutojaza takwimu sahihi na kushindwa kuwahudumia wananchi kwa wakati.

Amesema Serikali baada ya kuona changamoto hiyo imejiwekea mikakati ya kumsaidia mtumishi wa ngazi ya zahanati kutumia TEHAMA katika ukusanyaji, utunzaji na utumiaji wa takwimu sahihi katika kufanya maamuzi.

 “Imekuwa ni utaratibu wa Mtumishi wa afya ngazi ya nchini kuwa na fomu nyingi za kujaza (mfano mtua) hivyo serikali iliamua kuingiza mifumo ya TEHAMA ambayo itakusanya taarifa zote na kuwa moja ili kumuwezesha mdau kuweza kupata takwimu zilizosahihi na kwa wakati za mgonjwa na mahitaji muhimu katika utoaji wa huduma” anasema Sultana.

Amesema kuwa lengo la kikao hicho ni kuwawezesha wadau kutoa changamoto zilizopo katika utoaji wa huduma katika ngazi ya Msingi ya utoaji huduma na kupendekeza jinsi ya kuboresha utoaji wa huduma za afya na kupunguza mizigo kwa watumishi.

Amesema kuwa kwa sasa serikali inampango wa kutoka katika matumizi ya karatasi na  kuingia katika matumizi ya TEHAMA hivyo kunatakiwa kuwa na Dira itakayosaidia kuonyesha muelekeo katika kufanya mabadiliko ya TEHAMA kwenye kutoa huduma za afya nchini

Aidha  amesema kuwa lengo kuu ni utoaji wa huduma bora kwa jamii, kuwa na takwimu sahihi na kwa wakati na kuingia katika mifumo ya TEHAMA  kutoa huduma sahihi na upatikanaji wa takwimu sahihi.

“Unakuta mtumishi wa afya katika ngazi ya Zahanati anahudumia mteja huku ukijaza fomu mbalimbali kwa ajili ya kuweka rekodi jambo ambalo linasababisha kutokuwa makini na ujazaji wa takwimu na kushindwa kuweka kumbukumbu sahihi.

Aidha amesema kuwa Mifumo ya TEHAMA itasaidia utoaji wa taarifa sahihi na kwa wakati , upatikanaji wa taarifa ya mgonjwa popote pale nchini kwa urahisi.

Naye Mkurugenzi Msaidizi Huduma za Ustawi wa Jamii, Idara ya afya, Ustawi wa Jamii na lishe kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Bw. Rasheed Maftah amesema kwa sasa TAMISEMI ipo katika hatua ya kuboresha huduma za afya ya msingi kwenye Mamlaka za Serikali za mitaa.

Anafafanua zaidi na kusema kuwa moja ya hatua ya msingi ni  kuimarisha huduma za afya kuanzia ngazi ya Zahanati kwa kuimarisha mifumo ya TEHAMA ili kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma za afya kwa jamii.

Bw. Maftaa amesema kuwa Mpango wa kuboresha Matumizi ya Takwimu za Afya (Data Use Partinership –DUP)ulianza na mchakato wa kupata maeneo ya  kimkakati ya uwekezaji na baada  ya kupatikana ndipo utekelezaji ulipoanza ambapo kwa sasa upo katika hatua ya awali ya utekelezaji.

Aidha amesema sema Mpango huo utasaidia Mamlaka za Serikali za Mitaa kuongeza ufanisi na  ubora wa utoaji huduma kwa wananchi hususani katika Zahanati na vituo vya afya,  kuboresha miundombinu ya TEHAMA, kuawajengea uwezo watumishi  na kubadilisha mifumo ya awali iliyokuwa ikifanyika kwa njia ya karatasi  na kuingiza mifumo hiyo katika TEHAMA



Announcements

  • Call for applications for the TDR Postgraduate Training Scholarship in Implementation Science for the 2022 Academic Year (starting January 2022) May 16, 2021
  • Free Online IMF-Public Financial Management Course May 18, 2021
  • ARISE-PP Grants: Call for Expressions of Interest June 25, 2021
  • APPLICATION FOR THE SWEEDEN 2021 SCHOLARSHIP PROGRAM IS OUT. July 12, 2021
  • View All

Latest News

  • TUNZENI VIFAA VYA AFYA VILIVYONUNULIWA NA SERIKALI - DKT. MAHERA

    March 30, 2023
  • WAUGUZI NA WAKUNGA WATAKIWA KUSIMAMIA MAADILI YA KAZI

    March 13, 2023
  • DKT. DUGANGE AAGIZA UCHUNGUZI KUFANYIKA HOSPITALI YA WILAYA ARUSHA, UPOTEVU WA MAPATO NA DAWA

    March 08, 2023
  • SERIKALI KUSOGEZA HUDUMA ZA AFYA TARAFA ZOTE

    March 02, 2023
  • View All

Video

Hospitali ya Uhuru Dodoma
More Videos

Quick Links

  • elearning.moh.go.tz
  • About Us

Related Links

  • Line ministry
  • Regions
  • Councils
  • Development partners
  • Institutions & Agences
  • Development Partners Group Tanzania (DPG)

World visitors tracker

world map hits counter

Contact us

    PO-RALG

    Postal Address: 1923

    Telephone: +255 26 232 1 234

    Mobile: +255 735160210

    Email: james.tumaini@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

Writingmasterthesis.com

    • FAQ
    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.